Latest Posts

    Thursday, 21 August 2014

    CONTACT TO SUPER SKILLS FC


    LOCATION:
    KIMRA BARUTI

    CONTACT:
    supersskillsfootballclub@gmail.com

    MOBILE:
    0785 361 334
    0654 291 932
    more »

    MATOKEO YA MCHEZO KATI YA SUPER SKILLS FC NA ANU STAR

    Club ya  Super skills football ya vijana walio na umri chini ya miaka 14, ambayo Inapatikana Kimara Baruti Mtaa wa Kwa mtabili. Ilitolewa katika michuano ya CHAMPION CUP Katika mchezo wa fainali uliyozikutanisha kati yao na mahasimu wao wakubwa ANU STAR Baada ya kuchapwa bao 1-0. Mashindano hayo yaliandaliwa na UONGOZI wa CHAMPION FC.Mashindano hayo yalikuwa maalum kwa wachezaji walio na  umri chini ya miaka 14.


    more »

    Monday, 18 August 2014

    FIFA KUBORESHA MAKAO MAKUU YA TFF


    Shirikisho la Mpira wa Miguu duniani (FIFA) limeahidi kuboresha makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) yaliyoko kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala ili yawe katika kiwango cha kisasa ikiwa ni pamoja na kuwa na vitendea kazi na miundombinu ikiwa ni pamoja na upanuzi wa ofisi.

    Hatua hiyo itaiwezesha TFF kuwa na mazingira bora ya
    kufanya shughuli zake kwa ufanisi.


    Vilevile kupitia programu zake mbalimbali ikiwemo ile ya Goal, FIFA imeahidi
    kushirikiana na TFF katika kuendeleza mradi wa kiuchumi kwenye Uwanja wa
    Kumbukumbu ya Karume.


    Mwanzoni mwa mwaka huu, TFF ilihamishia makao yake makuu katikati ya
    jiji ili kupisha maendeleo ya kuiwezesha Karume kuwa kituo cha kisasa kwa
    michezo na vitega uchumi.


    Akiongea mwishoni mwa ziara ya kikazi nchini, Meneja Miradi wa FIFA
    anayeshughulikia Programu za Afrika, Zelkifli Ngoufonja amesema
    FIFA inaunga mkono wazo la kuboresha makao makuu ya Karume na itasaidia
    kwa awamu uboreshaji huo.


    Katika kuhakikisha usimamizi na utekelezaji
    barabara wa mradi huo, ujumbe huo wa FIFA ulikubaliana na Kamati ya
    Utendaji ya TFF kuboresha ofisi za Karume ili jengo la utawala lianze
    kutumika huku mradi ukitekelezwa kwa awamu.




    Pamoja na kuongelea mradi huo muhimu kimichezo na kibiashara, ujumbe huo uliokuwa nchini kwa juma moja kufuatia mwaliko wa TFF ulikuwa na nafasi ya kujadiliana na TFF kuhusu maboresho katika masuala mbalimbali yakiwemo ya Utawala, Fedha, Masoko, Ufundi, Mashindano na timu za taifa.






    Akiongea kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya TFF, Rais wa TFF Jamal Malinzi
    aliushukuru ujumbe huo wa FIFA kwa msaada mkubwa katika historia ya
    mahusiano kati ya FIFA na TFF.


    Ujio huo unafuatia maombi ya TFF kuwa sehemu ya mradi wa Performance wa
    FIFA. Mradi wa Performance unaoshirikisha nchi
    mashirikisho 163 kati ya wanachama 209 wa FIFA, unalenga kuongeza ufanisi
    katika uendeshaji na uongozi wa nchi wanachama wa FIFA.




    SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
    more »

    ARSENAL NA MANCHESTA UNITED WAKIMTAKA DOUGLAS COSTA WANAPASWA KUWEKA MKWANJA MEZANI PAUND MILLIONI 40



    Douglas Costa (kulia) nafukuziwa na Manchester United na Arsenal

    Arsenal na Manchester United wameambiwa waziwazi kuwa wanapaswa kupandisha dau mpaka kufikia pauni milioni £40 endapo kweli wanataka kumsajili Douglas Costa kutoka Shakhtar Donetsk.


    Costa mwenye umri wa miaka 23 amekuwa akihusishwa na kuondoka Shakhtar wiki zijazo kufuatia kugomea kurejea Ukraine kwasababu ya matatizo ya kisiasa.


    Uwezo wake aliouonyesha katika klabu ya Shakhtar umepelekea vilabu vingi barani Ulaya vikiwemo Arsenal na AC Milan ambavyo vimekuwa vikipimana ubavu kudaka saini ya Mbrazil huyo.


    Taarifa kupitia gazeti la Daily Stars zimearifu kuwa mashetani wekundu watapaswa kuongeza dau lao mpaka kufikia pauni milioni £40 ili aweze kutua Emirate Stadium msimu huu wa kiangazi huku mabosi wa klabu yake wakisema mshambuliaji huyo ni bora zaidi ya mwenzake Hulk.


    Mchezaji mwenyewe anataka zaidi kuelekea Arsenal kuliko kujiunga na United.
    more »

    YANGA NA SIMBA ZAZIDIWA KETE NA COASTAL UNION YA TANGA



    Ramadhani Salum Mohamed

    UONGOZI wa Klabu ya Coastal Union ya Tanga umeizidi kete klabu ya
    Simba SC baada ya kumsajili kiungo kati wa timu ya Gormahia ya nchini
    Kenya,Rama Saluma Mohamed aliyekuwa akiwaniwa na klabu hiyo.

    Rama ametua kwenye klabu ya Coastal Union akitokea nchini Kenya
    na kusaini mkataba wa kuitumikia timu hiyo kwa kipindi cha mwaka
    mmoja.

    Rama aliyewahi kuicheza timu hiyo kwa mafanikio makubwa na kufanikiwa
    kupata namba kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Kenya Harembee Stars
    alitua jijini Tanga juzi usiku akiwa na kulakiwa na viongozi wa klabu
    hiyo.

    Akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye makao makuu ya Klabu
    hiyo barabara 11,Katibu wa Coastal Union,Kassim El Siagi amesema
    kikosi cha cha timu hiyo msimu ujao kinatarajiwa kuwa tishio kutokana
    na kufanya usajili wa nguvu ambao unaonekana utaleta
    upinzani mkubwa sana.

    Aidha amesema kikosi chetu msimu ujao kitakuwa tishio kwa
    sababu tunamatumaini makubwa ya kufanya vizuri kutokana na usajili
    imara ambao tumeufanya kwa kusajlili wachezaji nyota kama vile
    Obina,Shabani Kado Sued Tumba ,Bakari Mtama, na wengine wengi walipokwenye kikosi cha timu hiyo

    Amesema bado wanaendelea na mchakato wa kuhakikisha wanaimarisha
    kikosi hicho kwa ajili ya maandalizi ya kuelekea msimu mpya wa ligi
    kuu Tanzania bara msimu ujao.
    Mwisho.
    more »

    Wednesday, 13 August 2014

    VAN GAAL AWAOMBA SUBIRA MASHABIKI WA UNITED.


    MENEJA mpya wa Manchester United Louis van Gaal anadhani atahitaji muda zaidi ili kuibadilisha timu hiyo pamoja na kukamilisha mechi sitaza kujipia nguvu kabla ya kuanza kwa msimu kwa ushindi. United ilimaliza ratiba yao ya mechi zao kujipima nguvu kwa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Valencia jana usiku na kumpa Mholanzi huyo ambaye alichukua mikoba baada ya kuingoza nchi yake kushika nafasi ya tatu katika Kombe la Dunia, ushindi wa kwanza katika Uwanja wa Old Trafford. Sasa United wanakabiliwa na mchezo dhidi ya Swansea City katika ufunguzi wa Ligi Kuu nyumbani Jumamosi lakini Van Gaal hana uhakika kama Jonny Evans, Luke Shaw na Antonio Valencia ambao hawakucheza mechi ya jana kutokana na majeruhi kama watakuwa fiti. Watatu hao wakiwa benchi, Van Gaal alilazimika kuwatumia Phil Jones, Chris Smalling na Tyler Blackett katika nafasi ya ulinzi wa kati huku Asley Young na Reece James wakicheza kama katika wingi. Akiwa amefanikiwa kufanya usajili wa wachezaji wawili pekee ambao ni Shaw na Ander Herrera kiangazi hiki, Van Gaal amesema bado anahitaji muda kwani timu wala wachezaji hawawezi kubadilika katika kipindi cha wiki mbili au tatu.
    more »

    TFF YAKANA KUTAMBUA UONGOZI MPYA COASTAL UNION.

     
    SHIRIKISHO la Soka wa nchini-TFF limedai kutotambua mabadiliko ya uongozi ndani ya Coastal Union yanayodaiwa kufanywa na mkutano wa wanachama wa klabu hiyo uliofanyika hivi karibuni. Katika taarifa ya shirikisho hilo iliyotumwa na Ofisa Habari wake Boniface Wambura, TFF imesema wao wanatambua uongozi wa Coastal Union uliochaguliwa na mkutano wa uchaguzi wa klabu na ndio wataendelea kufanya nao kazi, na sio uongozi mwingine wowote ule. Shirikisho hilo limewakumbusha wanachama wakewakiwemo Coastal Union kuheshimu katiba ya TFF pamoja na katiba zao, kwani hazitambui mapinduzi ya uongozi wala kamati za muda za utendaji. TFF inafanya kazi za kamati za utendaji zilizopatikana kwa njia ya uchaguzi tu. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa tayari TFF imepokea barua kutoka kwa Kaimu Mwenyekiti wa Coastal Union, Steven Mnguto ikilalamikia kusimamishwa kwake na wanalifuatilia suala hilo kwa kina, na ikibainika kuwa kuna viongozi wamehusika katika mapinduzi hayo watafikishwa katika vyombo husika kwa hatua zaidi.
    more »

    ATSU ATUA RASMI EVERTON.


    MENEJA wa klabu ya Everton, Roberto Martinez amesema dili la kumsajili winga wa kimataifa wa Ghana Christian Atsu kutoka Chelsea limekamilika. Atsu ambaye alikuwemo katika michuano ya Kombe la Dunia, msimu uliopita alicheza kwa mkopo katika klabu ya Vitesse Arnhem ya Uholanzi na sasa amekubali kwenda tena kwa mkopo Everton. Akizungumza katika shughuli ya uzinduzi wa msimu mpya wa Ligi Kuu nchini Uingereza leo, Martinez amesema anamtegemea Atsu kujiunga nao kesho kwasababu kila kitu kimeshakamilika na Chelsea. Atsu mwenye umri wa miaka 22 ataungana na Romelo Lukaku ambaye naye alitokea Chelsea na kutua Goodison Park huku mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji akiigharimu Everton paundi milioni 28.
    more »

    WAYNE ROONEY ACHAGULIWA KUWA KEPTENI MPYA WA TIMU YA MAN UNITED


    MANCHESTER UNITED imemteua Wayne Rooney kuwa ndie Kepteni wao mpya.
    Rooney, Miaka 28, anachukua wadhifa uliokuwa ukishikiliwa na Nemanja Vidic ambae amemaliza Mkataba wake na kuhamia Inter Milan Mwezi uliopita.
    Klabu hiyo pia imemteua Darren Fletcher kuwa Msaidizi wa Rooney.
    Jana, wakicheza Mechi ya Kirafiki na Valencia Uwanjani Old Trafford na kushinda 2-1, Rooney ndie alivaa utepe wa Nahodha na Jumamosi Agosti 16 ataiongoza Man United hapo hapo Old Trafford kwenye Mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu England Msimu mpya wa 2014/15 dhidi ya Swansea City.
    Akiongea baada ya kuteuliwa, Rooney alisema: “Hii ni heshima kubwa mno na nitatumikia kwa fahari kubwa. Namshukuru sana Meneja kwa imani yake aliyoonyesha kwangu.”
    Rooney, alieanzia Soka lake huko Everton, ameshawahi kuwa Nahodha kwenye Mechi kadhaa huko nyuma.
    Akiwa na Man United, Rooney ameshatwaa Ubingwa wa England mara 5, UEFA CHAMPIONS LIGI Mwaka 2008 na hivi sasa anashika Nambari 3, nyuma ya Sir Bobby Charlton na Denis Law, katika Ufungaji bora wa Magoli katika Historia ya Man United akiwa na Mabao 216.
    Ingawa wengi walitarajia Meneja Louis van Gaal atamteua Robin van Persie kuwa Nahodha hasa kwa vile ndie alikuwa Nahodha wa Netherlands wakati Van Gaal akiwa Kocha Mkuu wa Nchi hiyo na urahimu na ukaribu wao, Meneja huyo amemchukua Rooney kutokana na kuwa Mchezaji mzoefu wa muda mrefu hapo Old Trafford.
    Rooney alijiunga na Man United Mwaka 2004.
    Akiongelea uteuzi huu, Van Gaal alisema: “Kwangu mimi ni muhimu sana uchaguzi wa Kepteni. Wayne ameonyesha mfano mzuri sana kwa kila analofanya. Nimevutiwa sana na kazi yake na ari yake Mazoezini na kwenye falsafa yangu.”
    Kabla ya Nemanja Vidic kuwa Nahodha, Gary Neville ndio alioshika wadhifa huo na Wakongwe wengine, ambao ni Malejendari, walioshika Nafasi hiyo ni kina Sir Bobby Charlton, Bryan Robson, Eric Cantona na Roy Keane.
    more »

    KWANINI VILABU VYA TANZANIA VINAFUKUZA MAKOCHA ??



    Mpenzi msomaji wa Kurasa hii karibu tena kwa safu yangu leo nimeona tuangazie sakata kubwa ambalo linaonekana kushtua mioyo ya watu wengi Nchini Tanzania . Kuna msemo mkubwa unaosema makocha huajiriwa ili wafukuzwe yamekuwa ni mazoea kuutumia msemo huu Sehemu Kadhaa lakini naomba tutazame kwa kina kwanini makocha wa wanaokuja Tanzania huishia kufukuzwa ?


    Msimu wa mwaka 2013/14 katika timu kumi na nne ni makocha wawili tu ndio walio dumu kufundisha timu zao za ligi kuu Juma mwambusi Mbeya city na Mecky Mexime Mtibwa sukari makocha waliosalia wote walifukuzwa kwa maana walioanza sio waliomaliza ! Labda la kwanza tutazame kwanini yanatokea haya . timu ya soka ya Taifa ya Tanzania imefundishwa na makocha wakuu wanne mpaka sasa Maximo,Jpoulsen,kim poulsen,na sasa Mart Noij wakiwa na wasaidizi wao tofauti na katika kipindi chote hicho klabu za Tanzania zimekuwa zikifundishwa na makocha tofauti tofauti na kwa maana hiyo hata wachezaji wamekuwa wakifundishwa farsafa tofauti kwa mara kadhaa .


    Ukitazama kwa upande wa mafanikio kwa makocha wote hao hakuna hata timu moja si klabu wa taifa Stars iliyofanikiwa katika hatua kubwa japokuwa Taifa stars iliishia kushiriki (chan) yaani mashindano ya mataifa ya afrika kwa wachezaji wa Ndani, Jambo ambalo sio la Kujivunia sana .Swali langu la msingi ni jambo gani kubwa hasa au kwanini makocha wanafukuzwa kila kukicha na wengine wakirejea kufundisha klabu walizofukuzwa mara kadhaa .tunachogundua hapa ni kuwa lazima tujiulize maswali ya msingi makocha hawajui kufundisha ? je wachezaji wetu wanaelewa? kwanini iwe makocha ndio wanaukuzwa kila siku na sio wachezaji


    kwa miaka zaidi kumi hakuna hata timu hata moja ya Tanzania iliyofanya jambo la maana katika mashindano ya kimataifa na mafanikio yao makubwa yamekuwa ni kutwaa ubingwa wa Tanzania tu na wakijitahidi Ubingwa wa Cecafa je kuna shida gani na sio Tanzania hata afrika mashariki tunatatizo hilo je kuna tatizo gani?


    Pengine yafuatayo yanaweza kuwa sababu uelewa Mdogo wa wachezaji husika pindi wawapo mazoezini na kusingizia mazoezi magumu kumpakazia kuwa kocha ni mkali au anatukana lakini kuna kocha asiyetukana kiwanjani ? yapo mambo mengi ambayo makocha wa kigeni wanapokuja hutaka kutuletea kwenye mstari lakini hushindikanika kwa sababu ya tabia zetu mbaya za ukaidi je unafikiri hawa makocha tunaowafukuza wanaizungumziaje Tanzania pindi wawapo makwao je mchezaji wa kitanzania anapokwenda kujaribu soka ulaya unafikiri kwanini wanashindwa kwasababu wanafanya upembuzi kukujueni tabia zenu kiukweli tutafukuza makocha mpaka mwisho wa Dunia na hatutofanikwa kamwe kushinda chochote kwa sababu ya kuwalea watoto kama yai katika soka sio Jambo rahisi hata kidogo.


    Hari iliyopo sasa lazima tutawaona makocha hawajui kufundisha na tutasingizia vitu vingi sana lakini jambo la msingi ni kuu je wachezaji hawa wanafundishika na hapo ndipo utakapoona kuwa mfumo mzima wa soka la Tanzania una matatizo makubwa na haijulikani yatakwisha lini .
    more »

    Tuesday, 12 August 2014

    MARCIO MAXIMO KUINOA YANGA SANA KWA MARA YA KWANZA.




    Kocha Marcio Maximo aliechukua mikoba ya kuifundisha timu ya Yanga, ataanza na kibarua cha michuano ya Kagame, ambayo itafanyika huko Rwanda kuanzia Tarehe 8 mwezi wa Nane.

    Yanga ipo kundi A, na itaanza na Rayon. Katika kundi hilo ipo pia KMKM kutoka Zanzibar na Atlabara FC kutoka Sudani

    Washiriki pekee kutoka Tanzania ni KMKM na Yanga SC
    more »

    SASA RIHANNA KUWEKA OFA MEZANI KUINUNUA LIVERPOOL USHAURI KUTOKA KWA DROGBA



    Rihanna anajipanga kuonyesha mapenzi yake mapya katika mchezo wa mpira ambapo sasa ana elekea kuzindua mpango mpya kuinunua klabu ya Liverpool.

    Malkia huyo wa muziki wa Pop aliteka nyoyo za watu katika kombe la dunia nchini Brazil, alipokuwa akionekana kuchanganywa na matukio ya michezo ya fainali hizo.

    Taarifa zinasema kuwa msanii huyu amekuwa akitaka kuwekeza katika klabu ya nchini England huku gazeti la El Mundo Deportivo likiarifu kuwa Liverpool ndio chaguo lake.

    Gazeti hilo limearifu kuwa Rihanna ameshauriwa na rafiki yake wa karibu ambaye ni mshambuliaji wa Chelsea Didier Drogba kuweka ofa yake Anfield.


    Huyu ni Rihanna akichizika na soka .
    more »
    © 2013 SUPER SKILLS FC. WP Theme-junkie converted by Bloggertheme9